Mkuu wa Wilaya ya Temeke Godwin Gondwe amempa Mkandarasi siku saba arekebishe Barabara ya Keko

Mkuu wa Wilaya ya Temeke Godwin Gondwe amempa Mkandarasi siku saba arekebishe Barabara ya Keko ambayo imekuwa kero ya muda mrefu kwa Wakazi wa Temeke.

“Hii ni Barabara ambayo ipo kwenye mpango wa kupita magari yaendayo kasi, moja ya makubaliano katika mkataba ni kufanya marekebisho madogomadogo na tayari TANROADS wamewakabidhi, hatuwezi kukaa kusubiri, nimewapa siku saba Wakandarsi watengeneze ili Wananchi wa Temeke waendelee na kazi zao”-Gondwe

“Magari yanaharibika, madereva wanafukuzwa kazi na Maboss wao wanasema spring zinaharibika, wanachelewa kazini ubovu huu wa Barabaea ndio unawachelewesha, TANROADS wameshawaandikia barua nimewaleta waone kero wanayopata Wananchi mpaka Alhamisi Barabara ipitikeā€- Gondwe