Habari Kwa Picha Rais Magufuli aongoza waombolezaji kuaga mwili wa Katibu Mkuu kiongozi John Kijazi Viwanja vya Karimjee

Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam kwenye shughuli ya kuaga mwili wa aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Mhandisi John William Kijazi. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli atawaongoza waombolezaji katika kutoa heshima za mwisho kwa marehemu

“Kijazi alikuwa hajikwezi, Mimi ananizidi umri amezaliwa 1956 na Mimi 1959 ila ukimuita alikuwa mnyenyekevu sana, hakuwa na makuu, saa nyingine ukitaka kumtumbua Mtu anakuambia subiri hata siku mbili uangalie, wapo wengine wamesurvive kwasababu ya Kijazi”- JPM
“Kijazi alizaliwa 1956 ila bado alikuwa Katibu Mkuu Kiongozi, maana yake ulipofika wakati wa kustaafu mwaka 2017 nikajaribu kutafuta wa kuchukua nafasi yake nikakosa, nikamuongeza miaka miwili ikaisha sikupata, nikamuongeza mingine miwili, Mungu akasema ngoja akamtumie yeye”