JK NDANI YA MKASI

“Nilienda shule mara ya kwanza Lushoto mwaka 1956, nilikuwa napenda kucheza sana, mwalimu akasema kesho usije shule nikaona sawasawa tu. Rafiki yangu yeye alikuwa hajaanza nikaacha shule mpaka niliporudi tena” – Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

“Ni kweli kwamba watu wetu hawasomi sana, hata magazeti wanasoma vichwa vya habari tu. Mimi nilijua kusoma na kuandika baada ya kwenda shule” – Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

“Nilipomaliza Sekondari nikaenda Kibaha Form 5 na 6 baada ya hapo nikaenda Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 1975” – Rais Mstaafu Jakaya Kikwete

“Mke wangu wa kwanza mama yao wakina Ridhiwan, Mungu amrehemu. Ilikuwa siku moja tumetoka na baba tukaingia nyumba 1 tukamkuta msichana tukabaki tunatazamana tu. Tulivyorudi baba akasema umemuonaje yule msichana” – Rais Mstaafu Jakaya Kikwete