CHINA IMEFANIKIWA KUWASILISHA CHOMBO CHAKE MWEZINI

Kinalenga kukusanya mawe na mchanga kilo mbili ili kuleta duniani

Kinalenga kukusanya mawe na mchanga kilo mbili ili kuleta duniani

Chombo kilichotumwa mwezini na China kwa lengo la kukusanya mawe na mchanga chawasili

Taifa la China limefanikiwa kuwasilisha chombo cha change e-5 cha anga za mbali katika mwezi.

Picha zilizopigwa zilitolewa huku chombo kimoja kikionekana kivuli chake katika sakafu hiyo yenye vumbi jingi.

Chombo hicho kwa jina Change e-5 mission kiliwasili katika sakafu ya mwezi muda mfupi uliopita kwa lengo la kukusanya sampuli za mawe na vumbi ili kuleta duniani.

Mpango huo ulilenga eneo moja lenye volkano karibu na eneo kwa jina Oceanus Procellanum .

Chombo hicho kinatarajiwa kusalia huko kwa siku chache zijazo kikichunguza mazingira na kukusanya mawe hayo na vumbi lililopo.

Kina vifaa kadhaa ikiwemo kamera rada na kijiko na kifaa cha kuchimba .

lengo ni kukusanya takriban kilo 2 za mchanga na kutuma katika kifaa ambacho kinaweza kuwasilisha bidhaa hizo duniani.

Ni takriban miaka 44 tangu hatua kama hiyo kuchukuliwa .

Ikilinganishwa na uzinduzi wa chombo hicho duniani wiki moja iliopita kuwasili kwake katika mwezi hakukuangaziwa mubashara na runinga za China.

Muda tu baada ya chombo hicho kuwasili katika sakafu na kuthibitishwa ndiposa walipotangaza mafanikio hayo.