
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt Hussein Ally Mwinyi amefanya uteuzi Wakuu wa Mikoa kama ifuatavyo :
- Idrissa Kitwana Mustafa, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi.
- Ayoub Mohammed Mahmoud, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja.
- Rashid Hadid Rashid, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja.
- Salama Mbarouk Khatib, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba.
- Mattar Zahor Masoud, ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba.

You must be logged in to post a comment.