
Video ya Nyimbo ya ‘WAAH!’ ya Staa wa muziki wa BongoFleva Diamond Platnumz aliyomshirikisha Legend wa Muziki Barani Africa koffi olomide imeweka Rekodi Mpya Afrika Baada ya Kufikisha watazamaji Million 1 kwenye Mtandao wa YouTube ndani ya Masaa 8.
Video hii ambayo imeachiwa rasmi Leo Novemba 30, 2020 inamfanya Diamond Platnumz kuwa Msanii wa kwanza (Sub Saharan) Kufikisha Views Milioni 1 Ndani Ya Masaa 8 katika mtandao wa YouTube
Diamond amevunja Rekodi ambayo awali ilikua inashikirikwa na Davido ambae alifikisha Views Milion 1 ndani ya Masaa 9 kupitia Video yake ya .
Rekodi hii inaendelea kudhihirisha ubabe na nguvu kubwa aliyonayo Diamond katika Muziki, kwasababu si rahisi wala mzaha kufikia namba za kutisha namna hii!
You must be logged in to post a comment.