Wabunge wa Viti Maalum Chadema Waapa Majina yao haya hapa

Picha ya pamoja Spika wa Bunge, Mwanasheria mkuu wa Serikali na Wabunge wa Viti Maalum wa Chadema

Wabunge wa viti maalum kupitia chama cha upinzani cha CHADEMA wanaapishwa leo jijini Dodoma.

Wabunge hao 19 wameongozwa na Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chadema (Bawacha)Halima Mdee kula kiapo cha uaminifu mbele ya Spika Job Ndugai.

Awali, Chadema iligoma kuteua wabunge wa viti maalumu wakidai kuwa hawatambui matokeo ya uchaguzi uliopita wakisema ulikuwa na kasoro lukuki. Uongozi wa chama hicho ulidai kuwa na kutuma wabunge wa vti maalumu ni kuhalalisha uchaguzi huo.

Katika uchaguzi wa mwezi uliopita, Chadema ilipata mbunge mmoja tu wa kuchaguliwa jimboni, Bi Aida Kenani kutoka jimbo la Nkasi Kaskazini mkoani Katavi.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai amewaapisha Wabunge 19 wa Viti Maalum kutoka CHADEMA katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.
Walioapishwa ni;

  1. Mhe. Halima Mdee
  2. Mhe. Grace Tendega
  3. Mhe. Ester Matiko
  4. Mhe. Cecilia Pareso
  5. Mhe. Ester Bulaya
  6. Mhe. Agnesta Kaiza
  7. Mhe. Nusrat Hanje
  8. Mhe. Jesca Kishoa
  9. Mhe. Hawa Mwaifunga
  10. Mhe. Tunza Malapo
  11. Mhe. Felister Njau
  12. Mhe. Naghenjwa Kaboyoka
  13. Mhe. Sophia Mwakagenda
  14. Mhe. Kunti Majala
  15. Mhe. Stela Fiayo
  16. Mhe. Anatropia Theonest
  17. Mhe. Salome Makamba
  18. Mhe. Conchesta Rwamlaza
  19. Mhe.Asia Mohammed.