
Wafanyabiashara, wanafunzi na wasafiri wengine wanaovuka mpaka kutoka Uganda kuelekea Tanzania sasa wanaweza kusafiri kwa mabasi kama kawaida, limeripoti gazeti la Daily Monitor Uganda
Wafanyabiashara, wanafunzi na wasafiri wengine wanaovuka mpaka kutoka Uganda kuelekea Tanzania sasa wanaweza kusafiri kwa mabasi kama kawaida.
Usafiri wa basi ulikuwa umepigwa marufuku tangu mwezi Machi wakati serikali ya nchi hiyo ilipofunga mipaka yake na kupiga marufuku safari za umma ili kukabiliana na Covid-19, ambapo hadi sasa umekwisha wauwa watu zaidi ya140 nchini humo.
Wasafiri wanaoingia nchini Uganda hupitia mpaka wa Mutukula kwa kutumia mabasi yanayopita katika nchi za Tanzania, Burundi, Rwanda na Zambia.
You must be logged in to post a comment.